Tuesday, March 10, 2026

TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA MANISPAA MOROGORO

TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI

 

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro anapenda kuwatangazia
waombaji wote walioomba kazi ya Mtendaji wa Mtaa Daraja III kuwa Usaili utafanyika
tarehe 20 na 23 Juni, 2020 saa 1:00 asubuhi katika Chuo Kikuu Jordan (HEKIMA
HALL).
Aidha Usaili wa Mchujo (Written Interview) utafanyika tarehe 20/06/2020 na
wasailiwa watakaofaulu ndio watakaochaguliwa kuendelea na Usaili wa Mahojiano
(Oral Interview) tarehe 23/06/2020 katika Ukumbi wa Manispaa ya Morogoro siku ya
Jumanne kuanzia saa 1:00 Asubuhi.
Orodha ya waombaji walioitwa kwenye usaili ni kama inavyoonekana hapo chini, kwa
waombaji ambao majina yao hayakuonekana katika orodha hiyo watambue kuwa
maombi yao hayajakidhi sifa kwa mujibu wa nafasi zilizotangazwa. Mkurugenzi wa
Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro anawashukuru kwa kuleta maombi ya kazi
na wasisite kutuma maombi tena kipindi Halmashauri itakapotangaza nafasi za kazi
ambazo zitaendana na sifa walionazo.
Waombaji wote walioitwa kwenye usaili wanatakiwa kuzingatia maelekezo
yafuatayo:-

i. Wasailiwa wafike na Vyeti Halisi (Original) vya Taaluma, Kuzaliwa, Vyeti vya
Shule na Kitambulisho.

ii. Vitambulisho vitakavyokubaliwa ni pamoja na Kitambulisho cha Uraia,
kitambulisho cha Kupiga Kura, Leseni ya Udereva au Pasi ya Kusafiria.
2

iii. Kwa waombaji waliosoma nje ya Tanzania wahakikishe Vyeti vyao
vimehakikiwa na kuidhinishwa na Mamlaka husika (TCU, NACTE na
NECTA).

iv. Msailiwa anayekuja kufanya usaili atajigharamia mwenyewe

v. Msailiwa anatakiwa kuzingatia tarehe, muda na eneo la usaili

vi. Usaili utafanyika kwa njia ya maandishi na mahojiano

vii. Kila msailiwa anatakiwa kufika kwenye eneo la usaili akiwa amevaa
Barakoa (Mask) na kuzingatia maelekezo yote ya kujikinga na Corona.

viii. Tahadhari usaili utafanyika kwa mujibu wa Sheria, Taratibu na Kanuni za
Utumishi wa Umma, kuna matapeli wanaotumia majina ya watu na vyeo vya
watu kwa lengo la kujipatia fedha kuweni makini na matapeli hao. OFISI

HAITAWASILIANA NA MSAILIWA YEYOTE KWA NJIA YA SIMU

 

MAJINA // TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI

Hot this week

NGAZI NA VIWANGO VYA MISHAHARA SERIKALINI | Public Servant Salary Scales – Tanzania

In 2014 , the Government implemented new Salary Scales,...

Community Growth Manager- Remote

Responsibilities We are seeking passionate, dedicated people to join as Community...

PROCEDURES AND REQUIREMENTS ON HOW TO GET TANZANIA PASSPORTS AND TRAVEL DOCUMENTS

Tanzania government issues various types of passports and other...

UNIVERSITY OF EDINBURGH JULIUS NYERERE MASTERS SCHOLARSHIPS 2025 FOR TANZANIANS TO STUDY IN THE UK (FUNDED)

Application Deadline:  28th January 2025.  Applications are now open for the...

Retail Sales Associate – Adidas

Full job description   RETAIL SALES ASSOCIATE Department: Retail Operations Direct Reporting Line:...

Digital Sales Representative required in South Africa

Full job description Job Overview Date Posted: Posted 7 days...

General Assistant – ADvTECH

Full job description The ADvTECH Schools Division leads the private...

MARKETING AND COMMUNITATIONS MANAGER, LALIGA SOUTH AFRICA (3363)

Full job description Are you interested in developing an international...

Central Data Capturer – Centurion – Ampath Laboratories

Full job description Advert Reference: P13870 Central Data Capturer - Centurion Job...

Apprenticeship (x40) – Afgri South Africa

Full job description AFGRI is offering an opportunity for an...

Related Articles

Popular Categories