TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI TANESCO Tar 20 – 23/6/2020

TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI


Katibu wa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma kwa niaba ya Shirika la
Umeme Tanzania (TANESCO) anapenda kuwataarifu Waombaji Kazi wote walioomba
kazi kuwa usaili unatarajiwa kuendeshwa kuanzia tarehe 20 hadi 23 Juni, 2020
nahatimaye kuwapangia vituo vya kazi waombaji kazi watakaofaulu usaili huo.
Wasailiwa wanaoitwa kwenye usaili wanapaswa kuzingatia maelekezo yafuatayo:-

i. Usaili utafanyika kuanzia tarehe 20 hadi 23 Juni, 2020 kama ilivyooneshwa
kwenye tangazo hili; muda na sehemu ambapo usaili utafanyika umeainishwa
kwa kila Kada;

ii. Kila Msailiwa anapaswa kunukuu kwa usahihi namba yake ya usaili wa mchujo
na kwa Madereva wenye usaili wa Vitendo pia, namba hizo zinapatikana kwenye
akaunti ya kila Msailiwa katika mfumo wa maombi ya kazi.

iii. Kila msailiwa anatakiwa kufika kwenye eneo la usaili akiwa amevaa
Barakoa (Mask);

iv. Kila Msailiwa anapaswa kuwa na kitambulisho kwa ajili ya utambuzi;
2

v. Vitambulisho vinavyokubalika ni pamoja na:- Kitambulisho cha Mkazi,
Kitambulisho cha Mpiga kura, Kitambulisho cha kazi, Kitambulisho cha Uraia au
Hati ya kusafiria;

vi. Wasailiwa wanatakiwa kufika na VYETI VYAO HALISI, kuanzia cheti cha
kuzaliwa, kidato cha IV, VI, Stashahada, Stashahada ya Juu, Shahada na
kuendelea kutegemeana na sifa za Mwombaji;

vii. Wasailiwa watakaowasilisha“Testimonials”, “Provisional Results”,
“Statement of results”, hatiza matokeo za kidato cha IV na VI (form V and
form VI results slips) HAVITAKUBALIWA NA HAWATARUHUSIWA
KUENDELEA NA USAILI;

viii. Kila msailiwa atajigharamia kwa Chakula, Usafiri na Malazi;

ix. Kila Msailiwa azingatie tarehe, muda na mahali alipopangiwa kufanyia usaili;

x. Kwa waombaji waliosoma nje ya Tanzania wahakikishe Vyeti vyao
vimehakikiwa nakuidhinishwa na Mamlaka husika (kama TCU, NACTE au
NECTA);

xi. Waombaji kazi ambao majina yao hayakuonekana katika tangazo hili
watambue kuwa hawakukidhi vigezo. Hivyo, wasisite kuomba tena pindi nafasi
za kazi zitakapotangazwa na kuzingatia mahitaji ya tangazo husika.

xii. Kwa kada ambazo wanatakiwa kusajiliwa na Bodi zao za Kitaaluma
wanapaswa kuja na vyeti vyao Halisi vya Usajili pamoja na Leseni
zakufanyia kazi.

 

MAJINA // TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI TANESCO

MAJINA // TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI TANESCO